Ufaransa Yapinga Matokeo ya Urais DRC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ufaransa Yapinga Matokeo ya Urais DRC
Ufaransa imepinga matokeo ya uchaguzi wa rais nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ikisema ushindi uliotangazwa kwa kiongozi wa upinzani, Felix Tshisekedi haulingani na matokeo ambayo mpinzani wake mkubwa, Martin Fayulu anaonekana kuupata.

Katika tamko lililotolewa jana baada ya matokeo ya awali kutangazwa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Yves Le Drian alisema Fayulu, ambaye alitangazwa kushika nafasi ya pili, ndiye aliyetakiwa kutangazwa mshindi.

"Kwa kweli inaonekana matokeo yaliyotangazwa, hayaendani na matokeo halisi," alisema alipozungumza na kituo cha televisheni cha CNews.

"Kwa kuangalia (matokeo halisi), Fayulu ndiye kiongozi aliyepatikana katika uchaguzi huu. "

Alisema Kanisa Katoliki, ambalo lina wafuasi wengi na ambalo lilituma waangalizi 40,000, linajua nani hasa aliyehinda na maoni yao yanaonyesha mshindi ni Fayulu.

"CENCO ilifanya ukaguzi na kutangaza matokeo ambayo yalikuwa tofauti," alisema akimaanisha baraza la maaskofu la Kanisa Katoliki.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad