Aristote Afunguka Bifu Lake na Irene Uwoya..Wadau Wamuita Yuda na Mnafiki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



SIKU chache baada ya habari kusambaa mitandaoni kuwa ana bifu kali na msanii wa filamu Bongo, Irene Uwoya huku chanzo kikidaiwa amekuwa akimsifia sana mpenzi mpya wa Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’, mpambaji maarufu wa wasanii wa kike, Aris Mwamtobe ‘Aristote’ ameibuka na kufungukia tofauti zao. 



Awali ilidaiwa kuwa, Uwoya ambaye alikuwa mteja mzuri wa saluni ya Aristote walikuwa kwenye bifu kali huku baadhi ya mashabiki wakimpa jina lingine Aristote la Yuda Msaliti ikiwa ni baada ya video kusambaa mitandaoni akimsifia mpenzi mpya wa Dogo Janja ambaye alikuwa mume wa staa huyo wa filamu.



Akizungumza na Risasi Jumamosi, Aristote alisema hana tatizo lolote na Uwoya kwa sababu alichokiongea kwenye video iliyosambaa ni kweli licha ya kwamba tangu iliposambaa msanii huyo hajafika tena kwenye saluni yake wakati ndiye staa aliyekuwa akitoa mkwanja mrefu kwa kujipamba.

 “Kiukweli sijisikii vizuri kabisa kupewa hayo majina (Yuda na mnafiki) nina watoto wanakua kesho wakisikia baba yenu alikuwa anaitwa Yuda yaani msaliti inakuwa haileti maana nzuri kabisa, lakini tangu hayo maneno yasambae mitandaoni hajawahi kuja hapa ofisini kwangu, zaidi ya kukutana naye tu mara moja.
“Pia isitoshe hii hainipunguzii kitu chochote kwa sababu naamini Uwoya siyo mtu wa kukaa na kinyongo muda mrefu, pia tatizo kubwa ni hawa wapambe ndiyo wanaomjaza maneno lakini yeye mwenyewe hana tatizo na mtu, ingawa mchumba wa Dogo Janja akija tena kutengeneza nywele dukani kwangu nitamsifia kama kawaida na Uwoya naye akija nitafanya hivyohivyo,” alisema Aristote.



Mpambaji huyo amejizolea umaarufu baada ya kuonekana akiwapamba mastaa wengi Bongo akiwemo Elizabeth Michael ‘Lulu’, Jacqueline Wolper, Rita Paulsen ‘Madam Ritha’ na wengineo huku akichombeza kwa kutaja maneno tofautofauti ya kuchekesha akiambatanisha na jina la ‘Aristoste mzee wa vikao’.

STORI: Memorise Richard, Dar es Salaam
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad