Mwigulu Nchemba Ataja Chanzo cha Ajali Aliyoipata

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mbunge wa Iramba Magharibi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Nchemba amesema kuwa ajali aliyoipata imesababishwa na Punda waliokuwa wakikatisha barabarani.

Ameyasema hayo katika hospitali ya Mkapa jijini Dodoma anakopatiwa matibabu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema kuwa alikuwa akitokea mkoani Iringa kuelekea mkoani Singida kuhudhuria kikao cha kamati ya siasa.

“Nilikuwa siangalii mbele kwa kuwa nilikuwa naongea na simu lakini ghafla nilishtushwa na tahadhari ya ajali niliyopewa na dareva wangu, nilipotazama mbele niliwaona punda watatu wanakatisha barabara na mmoja alifanikiwa kuvuka na kuwagonga wengine wawili. Nilichosikia ni sauti ya kishindo kikubwa kilichoashiria kuwa tumepata ajali, namshukuru Mungu ni mwema kwa kuwa ametuepusha na kifo,” Amesema Mwigulu

Aidha, amesema kuwa baada ya hapo aliona moshi umetanda ndani ya gari hali iliyoashiria gari hilo lingeweza kulipuka lakini wasamalia wema walifika na kuwaokoa na kuwawahisha hospitali ya Benjamin Mkapa.

Hata hivyo, mapema asubuhi ya leo taarifa za Mwigulu Nchemba kupata ajali zilisambaa huku chanzo kikiwa hakijatajwa mpaka pale alipozungumza mwenyewe.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad