Zaidi Ya Bil. 16.324.9 Zimelipwa Kwa Wakulima Wa Korosho Mkoani Pwani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Zaidi Ya Bil. 16.324.9 Zimelipwa Kwa Wakulima Wa Korosho Mkoani Pwani
JUMLA ya kilo 5,623,277 za korosho zenye thamani ya zaidi ya sh. bilioni 16.324.9 tayari zimelipwa kwa wakulima mkoani Pwani.

Aidha wakulima wa korosho 24,543 ,wenye kilo 14,370, 844 kati ya kilo 21,130,598 zilizopo kwenye maghala makuu wameshakikiwa, sawa na asilimia 68 .

Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Ndikilo alitoa taarifa hiyo wakati alipokuwa akizungumza kwenye ziara yake wilaya ya Mkuranga na Rufiji.

Alisema, zoezi la uhakiki lilikuwa mwisho february 15 lakini mkoa huo unaomba kuongezewa muda hadi february 28 mwaka huu, kwakuwa umechelewa kuanza zoezi hilo na bei ya daraja la pili ilichelewa kutoka ambayo itakuwa sh. 2,640 kwa kilo .

Ndikilo alieleza, hadi tarehe 12 februari, mwaka huu jumla ya kilo 23,066,238 za korosho zimekusanywa, ambapo kilo 21,130,598, sawa na asilimia 91.6 zipo kwenye maghala makuu.

"Ghala kuu la Mwanambaya zipo kilo 6,549,204, Kibiti kilo 2,650,529, TANITA kilo 1,705,621, Kurasini PISAH kilo 3,727,669, Kurasini SCALABLE kilo 6,325,237 ,Kiegeani- Mafia kilo 213,593 na kilo 6,488,690 zipo kwenye maghala madogo ya AMCOS"alibainisha Ndikilo.

Nae katibu tawala msaidizi uchumi na uzalishaji, Shangwe Twamala alisema mkoa wa Pwani ulichelewa kuanza ukusanyaji wa korosho tarehe 30 Oktoba, 2018 tofauti na mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma, ambayo ilianza mapema.

"Baadhi ya korosho kuendelea kuwepo kwenye maghala ya AMCOS, Ili kutatua changamoto hii, tunashauri malipo kwa wasafirishaji yafanyike kwa wakati ili waweze kufanya kazi hii"

"Kama itawezeakana tutumie magari ya jeshi kuhamisha korosho kutoka kwenye AMCOS kwenda maghala ya Kurasini"alieleza Twamala. Kwa upande wao mkuu wa wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga alisema, tani zaidi ya 4,000 za korosho kati ya 6,000 walizokusanya zipo chini ya sakafu ambapo wamezitandikia maturubai lakini wanahofia unyevunyevu zisije kuharibika.

Mkuu wa wilaya ya Rufiji Juma Njwayo alisema, wakulima wilayani hapo wamelipwa korosho sh. bilioni 3.7 ,kwa wakulima 2,665.#
Advertisement
advert
==



Advertisement
Usipitwe na Habari Yoyote. Install Mpekuzi App kwenye Simu Yako Upate Habari Zetu kwa Wepesi Zaidi

==>>... << BOFYA HAPA  Kui Install>>
==

Save On Electricity Costs With These 3 Tips Now
Womens Article
|
Sponsored
11 Cancer Symptoms You Are Probably Ignoring
Health & Human Research
|
Sponsored
World's Scariest Bridges
Viral X Files
|
Sponsored
7 Forbidden Destinations You Can Never Visit
Relocation Target
|
Sponsored
When You Eat 3 Dates Everyday For 1 Week This Is What Happens To Your Body
Food Prevent
|
Sponsored
11 Most Isolated Communities At The End Of The Earth
Relocation Target
|
Sponsored
The Foods To Eat To Prevent Cancer
Food Eat Safe
|
Sponsored
10 Easiest Countries for Immigration From Tanzania, United Republic Of
Immigration DO
|
Sponsored
.....


===
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )


Batuli 'Amwaga Machozi' Baada ya Picha zake za Nusu Uchi Kusambazwa MitandaoniMPEKUZI: Batuli 'Amwaga Machozi' Baada ya Picha zake za Nusu Uchi Kusambazwa Mitandaoni
Entertainment News,Politics News ,Celebrity Gossip and Live Updates,United States, United Kingdom Batuli  'Amwaga  Machozi'  Baada  ya  Picha  zake  za  Nusu  Uchi  Kusambazwa  Mitandaoni
MPEKUZI


Home
View web version

Wanafunzi 30 Wanusurika Kifo Dereva Akichat na SimuMPEKUZI: Wanafunzi 30 Wanusurika Kifo Dereva Akichat na Simu
Top 7 Bad Foods For Thyroid
Health & Human Research
|
Sponsored

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad