Abiria Wamchapa Dereva Kwa Uendeshaji Mbaya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Watu wanaosadikika kuwa ni abiria wa daladala, maarufu kama ‘matatu’ nchini Kenya, wamempiga dereva wa chombo hicho cha usafiri kwa madai kuwa uendeshaji wake haujali uhai wa abiria.

Video ya tukio hilo imesambaa kwenye mitandao ya kijamii hususan mtandao wa Twitter ambao ni maarufu zaidi nchini humo.

Matatu hiyo inamilikiwa na Lina Sacco ikiwa na nambari za usajili, KCL 740B, imeripotiwa kuwa ilikuwa ikitoka Limuru kuelekea Nairobi.

Abiria hao wameeleza kuchukizwa na tabia ya dereva huyo pamoja na rafiki yake walipokuwa barabarani na kwamba walionekana kutojali kabisa maisha yao.

Mmoja kati ya abiria alisikika akisema, “tumemkataza kukimbia, anataka kutuua kwa nini?”

Hivi karibuni kumekuwa na ripoti ya matukio mengi ya ajali za barabarani jijini Nairobi, hali ambayo imewafanya abiria kutowaamini madereva.

Kupitia mitandao ya kijamii, wengi wameonesha kuunga mkono kitendo cha abiria hao.

Jeshi la polisi jijini Nairobi limeeleza kuwa linafanya uchunguzi wa tukio hilo kwa kuanzia kwenye video iliyosambaa, huku ikionya wananchi kutojichukulia sheria mikononi.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad