AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa za ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa Atletico wamechoshwa na tabia zake ambazo zimekuwa zikiigharimu timu huku uwezo wake uwanjani ukiwa hauridhishi pia.
Msimu wa Costa kwa sasa umeshamalizika kwa kuwa amefungiwa kutocheza mechi nane kutokana na kumtukana mwamuzi katika mchezo dhidi ya Barcelona, mapema mwezi huu. Upande wa Simeone ameshikilia msimamo wake kuwa bado anamuhitaji mchezaji huyo licha ya kuwa amekuwa na matatizo kadhaa.
Costa alimtolea lugha kali mwamuzi, Gil Manzano huku akimshika na kumtikisa kwenye mikono, baada ya kupewa kadi nyekundu na timu yake ilifungwa mabao 2-0. Simeone hakumtetea Costa kwa kile alichokifanya lakini bado anaona ni mchezaji sahihi kuendelea kubaki kikosini hapo.
Hii ni mara ya pili Costa anaitumikia timu hiyo, awali aliondoka kwenda Chelsea lakini akarejea klabuni hapo kwa ada ya pauni 53m mwaka 2017. Amefunga mabao matano katika mechi 21 za michuano yote alizocheza
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK