"Niliumia Kuachana na Amini, Tunakuja" - Linnah

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

"Niliumia Kuachana na Amini, Tunakuja" - Linnah
Msanii wa Bongo Fleva, mwanadada Linnah amefunguka kuwa hakupenda kuachana na msanii Amini kwasababu alikuwa anampenda.

Linnah amesema hayo katika 'Interview' na Planet Bongo ya East Africa Radio, alipokuwa akitambulisha ngoma mpya aliyofanya pamoja na msanii huyo.

Alipoulizwa kuwa alijisikia vipi alipoachana na Amini, Linnah amesema, "kiukweli hakuna kitu kinauma kama kuachana na mtu unayempenda, mimi binafsi ninampenda Amini ndiyo maana niliumia".

"Hakuna asiyejua kuwa mimi na Amini tulikuwa wapenzi, kwahiyo watu wanaosema kuwa hivi sasa tumerudiana, hatuwezi kuwazuia kwa sababu wanapenda kutuona jinsi tulivyokuwa tukipendana", ameongeza.

Pia kuhusu uhusiano wa sasa baina ya wasanii hao ambao chimbuko lao ni THT, Linnah amesema kuwa atatafuta wakati rasmi wa kutambulisha penzi lao, lakini kwa sasa watambue tu kuwa wako pamoja na lolote linaweza kutokea.

Amini na Linnah kwa pamoja wametambulisha ngoma ya pamoja inayojulikana kama 'Nimenasa'.

Taarifa za kurejea kwa penzi la wawili hao lilianza kusambaa hivi karibuni, ikiwa ni baada ya Amini kuachana na mkewe na Linnah kuachana na baba wa mtoto wake hivi karibuni.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad