Korea Yamuua Mjumbe Wake Kisa Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Yorea Yamuua Mjumbe Wake Kisa Marekani
VYOMBO vya habari vya Korea Kusini hii leo vimeripoti kwamba Korea Kaskazini imemuua mjumbe wake maalumu kwa ajili ya Marekani Kim Hyok Chol kufuatia kushindwa kwa mkutano wa pili wa kilele kati ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un na Rais Donald Trump.

Gazeti la Chosun Ilbo limeandika Chol aliyeuandaa mkutano huo wa Hanoi na kumsindikiza Kim kwenye treni yake binafsi ameuawa kwa kupigwa risasi kwa kile kinachotajwa kumsaliti kiongozi huyo wa juu baada ya kufanikiwa kuishawishi Marekani wakati wa majadiliano ya kabla ya mkutano huo wa kilele.

Gazeti hilo lililonukuu chanzo ambacho hakikutambulishwa limesema Chol, aliuawa mwezi Machi, katika uwanja wa ndege wa Mirim pamoja na maafisa wanne waandamizi wa wizara ya mambo ya nje baada ya uchunguzi.

Mkalimani wa Kim kwenye Umoja wa Mataifa naye ametiwa kizuizini baada ya kufanya makosa kwenye mkutano huo wa kilele.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad