Koffi Olomide Azuiwa Kufanya Show Yake Afrika Kusini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kumbi mbili zimefuta tamasha za mwanamuziki wa Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo Koffi Olomide, ambaye hivi karibuni alipatikana na hatia ya kumbaka mmoja wa wasichana wanenguaji waliokuwa katika bendi yake wakati alipokuwa na umri wa miaka 15.

Olomide, mwenye umri wa miaka 62, ambaye jina lake halisi ni Antoine Agbepa Mumba, alitazamiwa kucheza muziki wake katika ukumbi wa Gallagher Convention Centre uliopo nje ya mji wa Johannesburg Juni 28 na katika Shimmy Beach Club mjini Cape Town siku mbili baadaye.

Lakini upinzani dhidi yake ulianza kupitia kampeni iliyoendeshwa kwenye mitandao ya habari ya kijamii kusitisha matamasha zake kutokana na kupatikana kwake na hatia ya ubakaji.

Marekani yatoa tahadhari nyengine Uganda
'Jeshi la polisi lilipata fununu za tishio la ugaidi kabla Ubalozi wa Marekani'
Makonda: Hakuna tishio Dar es Salaam
Marekani yakiri ndege yake kutunguliwa na Iran
"Tafadhari mnafahamishwa onyesho la Koffi Olomide ...halitafanyika ," alieleza mkurugenzi mkuu wa Convention Centre, Charles Wilson katika taarifa aliyoitoa Jumatano.

Shimmy Beach "ilifanya uamuzi wiki iliyopita wa kutokuwa mwenyeji wa tamasha la Koffi Olomide lililokuwa linaendeshwa na promota wa nje, kilisema kilabu kwenye ujumbe wake kupitia Twitter siku ya Jumanne.

Ruka ujumbe wa Twitter wa @ShimmyBeach

Shimmy Beach Club
@ShimmyBeach
 Please note that @ShimmyBeach will no longer be hosting Koffi Olomide. We made the decision to cancel the show last week.

40
1:18 PM - Jun 18, 2019
Twitter Ads info and privacy
49 people are talking about this
Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @ShimmyBeach
Taarifa ya kusitishwa kwa tamasha hilo iliafikiwa na baadhi ya watumiaji wa mtandao wa Tweeter waliokuwa wameanzisha kampeni ya kumzuwia kofi Olomide kufanya matamasha nchini Afrika Kusini chini ya #StopKoffiOlomide:

Ruka ujumbe wa Twitter wa @StopKoffiOlomi1

#StopKoffiOlomide
@StopKoffiOlomi1
 Yay! Good news! Gallagher Convention Centre has just confirmed to our campaign that the concert is not going ahead🎉🎈🎊

21
9:45 AM - Jun 19, 2019
Twitter Ads info and privacy
See #StopKoffiOlomide's other Tweets
Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @StopKoffiOlomi1
Mwezi Machi, mahakama ya Ufaransa ilimhukumu Bwana Olomide kifungo cha miaka miwili jela kilichoahirishwa baada ya kesi dhidi yake ambayo hakuidhuria.

Mahakama ya Nanterre, nje ya mji mkuu Paris, pia ilimuagiza alipe faini ya kiwango sawa kwa kuwasaidia wanawake watatu wengine kuingia nchini Ufaransa kwa njia haramu.

Wakili wa Olomidé alipongeza uamuzi huo na kuutaja kuwa ushindi, akiwaarifu waandishi habari kwamba uamuzi huo utachangia kuondolewa waranti ya kimataifa wa kumkamata.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad