Unaambiwa Watumiaji DAWA za Kulevya Wapungua Tanzania

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Tanzania imeungana na mataifa mengine duniani leo Juni 26, kuadhimisha siku ya kimataifa ya kupambana na matumizi na biashara ya dawa za kulevya, ikiwa ni nchi mwanachama wa umoja wa mataifa.

Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa mkoani Tanga yakiwa na kauli mbiu “Waathirika wa dawa za kulevya wana haki ya kupata huduma za afya” lengo likiwa ni kuikumbusha jamii juu ya uelewa wa wimbi la biashara na matumizi ya dawa za kulevya.

Kutokana na Serikali kuendelea kusimamia utoaji tiba kwa waathirika wa dawa za kulevya ili kupunguza madhara yanayotokana na matumizi ya dawa hizo, na kufanikiwa kupunguza idadi ya waathirika wa dawa za kulevya katika vituo vya tiba kutoka wagonjwa 2,400 mwaka 2015 hadi wagonjwa 700 mwaka 2018.

Hali iliyosaidia kupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa waraibu wa dawa za kulevya wanaojidunga kutoka 35% mwaka 2015 hadi 18.5% mwaka 2018.

Mbunge wa Kenya aliyetaka wafanyabiashara Watanzania wafukuzwe akamatwa
Ikumbukwe kuwa matumizi ya dawa za kulevya husababisha madhara kiafya ikiwa ni pamoja na kuchochea kuenea kwa maambukizi ya vurusi vya UKIMWI, virusi vya homa ya ini aina B na C,kifua kikuu, magonjwa ya akili pomoja na usugu wa tiba ya kifua kikuu.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad