AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imempa siku 7 mmiliki wa gazeti la Tanzanite, Cyprian Musiba na wachapishaji wa gazeti hilo kuwasilisha majibu dhidi ya madai ya Bernard Membe.
Waziri huyo mstaafu wa Mambo ya Nje anataka kulipwa Sh 10 bilioni kwa kuchafuliwa na gazeti tajwa.
Uamuzi huo wa mahakama umetolewa jana Jumanne Julai 2, mbele ya Jaji Joaquine Demelo baada kupitia maombi ya wajibu maombi ya kutaka waongezewe muda wa kuwasilisha utetezi na majibu kinzani.
Jaji Demelo alisema wajibu maombi walitakiwa kuwasilisha utetezi na majibu kinzani ndani ya siku 21 baada ya shauri kufunguliwa Desemba mwaka jana lakini hawakufanya hivyo ambapo Musiba kupitia Wakili wake Majura Magafu waliomba kuongezewa muda japo wadai walipinga maombi hayo wakitaka yasikubaliwe.
“Mahakama imesikiliza hoja za pande zote mbili imeona kesi ina maslahi kwa umma hivyo ni bora na upande mwingine wakasikilizwa.
"Hatuwezi kusikiliza shauri upande mmoja, kesi hii ina maslahi kwa umma kuna haja ya kuusikiliza na upande wa pili, nawapa siku saba muwasilishe utetezi na hati ya kiapo kinzani,” alisema Jaji Demelo.
Jaji Demelo alisema upande wa waleta maombi kama watakuwa na hoja za kujibu utetezi wawasilishe kabla ya Agosti 8, mwaka huu ambapo shauri hilo la madai litaanza kusikilizwa Agosti 6, mwaka huu.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Watanzania tuko nyuma ya Mheshimiwa Mwanaharakati Cyprian Musiba na SI Membe ambaye tayari anatoa harufu mbaya huku CCM.
ReplyDeleteAfyekwe uanachama.
UsirudieKosaKupigiaKuraUpinzaniOvyo!