Mkurugenzi wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Ajidhulu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Christine Lagarde ameondoka madarakani kama mkurugenzi wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).

Kuondoka kwake mamlakani kunakuja kabla ya uamuzi wa kuteuliwa kuwa mkuu wa benki Kuu ya Muungano wa Ulaya (ECB).

Bi Lagarde amesema kuwa ataondoka katika IMF tarehe 12 Septemba.

" Kwa uwazi uliopo sasa juu ya mchakato wa kuteuliwa kama rais wa Benki kuu ya Muungano wa Ulaya (ECB) na muda utakaochukua, lazima nichukue uamuzi kwa manufaa bora ya Shirika la fedha la kimataifa ," amesema.

" Mkurugenzi mtendaji wa bodi sasa atachukua hatua muhimu zinazohitajika kuendelea na mchakato ewa kumchagua mkurugenzi mpya."

Waziri huyo wa zamani wa Ufaransa amekuwa mkuu wa IMF tangu mwaka 2011.


Ikiwa baraza la Muungano wa Ulaya litaidhinisha uteuzi wake kuongoza ECB , atakuwa ni mwanamke wa kwanza kuwahi kuongoza benki hiyo ya Ulaya yenye jukumu la kuandaa sera ya sarafu ya Euro na masuala ya kifedha kwa ujumla katika nchi zinazotumia sarafu ya Euro.

Akifahamika kama "mwamba nyota" masuala ya fedha ya kimataifa , Bi Lagarde,mwenye umri wa miaka 63, alianza taaluma ya uwakili kabla ya kuingia katika masuala ya kisiasa.

Aihudumu kama waziri wa wizara kadhaa chini ya rais Nicolas Sarközy kabla ya kuchaguliwa kama Mkuu wa kwanza mwanamke wa IMF - akichukua nafasi ya Dominique Strauss Khan.

Je ni nani atayechukua nafasi ya Lagarde katika?

Uteuzi utaanza haraka. Lakini unaibua tena hoja ya mchakato wa zamani wa kumpata uongozi wa IMF na Benki ya dunia.

Kulikuwa na uelewa wa kipindi cha baada ya vita vya pili vya dunia - au dhana kwamba moja kwa moja mkuu wa IMF itachukuliwa na Mtu kutoka Ulaya huku, Marekani wakichukua nafasi ya Mkuu wa Benki ya dunia. Christine Lagarde aliendeleza utamaduni huo.

Alikuwa ni mkurugenzi mkuu wa 5 wa IMF kutoka taifa la Ufaransa. Suala hilo mara ya mwisho lilifichuliwa mapema mwaka huu, wakati nafasi ya kazi ilipojitokeza ghafla ya mkuu wa Benki ya Dunia.

Mtu aliyeteuliwa na rais Trump, David Malpass alipata kazi hiyo. Kumekuwa na changamoto juu ya utaratibu huo ulioanzishwa wa kuwapata wakuu wa mashirika hayo muhimu duniani.

Wakati Bi Lagarde alipochaguliwa, Mkuu wa benki kuu ya Mexicoce Agustin Carstens aligombea nagfasi hiyo dhidi yake na alikuwa hajawahi kuteuliwa mtu yeyote kutoka nje ya Ulaya kugombea wadhfa huo awali. Halitakuwa jambo la kushangaza ikiwa wagombea zaidi watajitokeza kugombea nafasi hiyo wakati huu. Hata hivyo kwa sasa vita vya mikataba ya baada ya vita vimesitishwa.

Mara nyingi, Bi Lagarde ambaye amekuwa akiwekwa juu katika orodha ya wanawake 10 wenye mamlaka zaidi duniani amesaidia ku jenga upya uaminifu kwa shirika la IMF baada Ugiriki kupewa dhamana mwaka 2010, ambayo ililegeza masharti ya IMF.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad