Ng'ombe Kupewa Cheti cha Kuzaliwa Uganda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Ng'ombe wote nchini Ugandan wanatarajiwa kupewa cheti cha kuzaliwa ili kufikia masharti ya kibiashara katika soko la Muungano wa Ulaya, EU.

Kwa mujibu wa Gazeti la Daily Monitor, Waziri wa kilimo, ufugaji na uvuvi Vincent Ssempijja amesema kuwa mataifa yanayokuza chakula kwa ajili ya soko la EU lazima yatoe stakabadhi inayo onesha bidhaa hiyo imetoka wapi.

Bw. Ssempijja aliongeza kuwa bidhaa kutoka Uganda zinashikiliwa au kupigwa marufuku Barani Ulaya.


"Wakulima watasajliliwa na bidhaa zao kupewa nambari maalum ili kurahisisha mchakato wa kibiashara kati nchi hiyo na mataifa mengine hasa yale ambayo ni wanachama wa Muungan wa Ulaya," alisema.

"Hatuwezi kunufaika katika masoko makubwa hadi wakulima wetu wasajiliwe ,"aliongeza.

Bw. Ssempijja amesema wakulima watasajiliwa kivyao na ng'ombe pia kupewa cheti cha kuzaliwa kwasababu waagizaji bidhaa za nyama wanahitaji nyama kutoka kwa ng'ombe waliona na miezi kati ya 15 hadi 24. Kwa hivyo tunauza bidhaa zetu kulingana na umri wao," alisema.

Kwa mujibu wa Bw. Ssempijja, kundi la washirikishi wa mpango huo kutoka Muungano wa Ulaya wanatarajiwa nchini Uganda mwezi Septemba mwaka huu ili kuhakikisha wakulima wanauza bidhaa zao katika soko la Ulaya wanafikia masharti hayo.

''Kando na kufahamu chanzo cha bidhaa wanazouziwa washirikishi hao pia wanataka kuhakikisha wakulima wananufaika moja kwa moja kutokana na biashara zao kwasababu wakati mwingine wanapujwa na wafanyibiashara walaghai.

Serilakali ya Uganda imetoa arifa kuwa haitafanya kazi na mkulima yeyote ambaye hata timiza masharti hayo.

Serikali pia imekanusha madai kuwa mpango huo unalenga kuwatoza wakulima ushuru wa zaida ambao uliondolewa Julai Mosi mwaka huu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad