AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wachezaji wawili wa timu ya Arsenal ya nchini England Sead Kolasinac na Mesut Ozil akiwa na mkewe, wamevamiwa jana kaskazini mwa Jiji la London na watu wawili waliokuwa na visu katika kile kilichoonekana kuwa tukio la ujambazi. Hata hivyo shukrani za pekee ziende kwa Kolasinac ambaye alipambana kuwaokoa jahazi.
Ozil alikuwa kwenye gari lake jeusi aina ya Mercedez kwenye makazi ya Kolasinac wakati watekaji hao walipojaribu kutekeleza jaribio hilo.
Katika picha ya video inayosambaa kupitia mtandao, Kolasinac anaonekana akipambana na wahalifu hao huku Ozil na mkewe wakiwa wamebaki kwenye gari.
Baadaye Kolasinac aliingia kwenye gari huku, wahalifu hao wakiwa bado wanaendelea kuwafuata kwa nyuma. Hata hivyo taarifa zinasema kuwa baadaye wahalifu hao waliondoka baada ya Kolasinac kuondoa gari kwa nguvu kwa nia ya kuwagonga.
Mpaka sasa, watu kadhaa wanashikiliwa kutokana na tukio hilo ambalo bado lipo chini ya uchunguzi. VIDEO:
Ozil gets robbed, kolasinac jumps out to batter absolute fuck out of the attackers, ozil drives away, kolasinac still continues to batter fuck out the attackers swinging knives at him, What a machine kolasinac is 😂😂 pic.twitter.com/uNRKztR803— Jack McDonald (@jackmcd976) July 26, 2019
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK