Tanasha ataja idadi ya ‘wapenzi’ wake kabla ya kukutana na Diamond

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Dar es Salaam. Tanasha Donna, mpenzi wa Diamond Platinumz  amesema hawezi kufuatilia wapenzi  wa zamani wa msanii  huyo wa Bongo Fleva kwa sababu kabla ya kuwa naye, alikuwa na uhusiano na wanaume watatu.


Kauli ya Tanasha imekuja siku kadhaa baada ya mpenzi wa zamani wa Diamond,  Zarina Hassan‘Zarithebosslady’ kumtakia kheri, kumtahadharisha ajipange kulea mtoto wake kutokana na aina ya baba aliyezaa naye ambaye ni Diamond.



 

“Siwezi kumlaumu kwa mahusiano yaliyopita kwani hata mimi kabla ya Diamond nilikuwa na wapenzi watatu, siyo shida na yeye akiwa nao, ”amesema mkali huyo wa wimbo 'Nah Easy'.


Amefafanua kuwa mpaka sasa hajaona tatizo lolote kwenye uhusiano wao, ndio maana hashughulishwi na mahusiano yaliyopita ya Diamond.



 

“Siwezi kumtilisha shaka kwa vitu alivyowafanyia wengine, namuangalia na kumpima mtu ninapokuwa naye binafsi, akifanya kitu tofauti na makubaliano yetu sawa, lakini sio kwa sababu aliwahi kuwafanyia wengine na mimi nipate hofu, ”amesema.


Mapema 2019,  Diamond aliwahi kummwagia sifa mrembo huyo kwamba ni mwanamke anayejielewa, anafanya vitu vyake kwa mpangilio, na hana muda wa kurushiana vijembe mtandaoni.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad