Marekani na Uchina mezani kutanzua mzozo wa kibiashara

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mataifa washirika wa Marekani wamemshinikiza Bwana Trump kumaliza vita na Uchina katika kikao cha G7 nchini Ufaransa , wakionya kuwa vita vya bishara vinatishia uchumi wa dunia
Rais Donald Trump amesema kuwa Marekani na Uchina zitafufua mazungumzo "muda mfupi sana ujao "baada ya kuongezeka zaidi kwa uhasama wa kibiashara na utawala wa Beijing mwishoni mwa Juma.

"China iliniita jana usiku ...Ikasema turejee tena kwenye meza ya mazungumzo . Kwa hiyo tutarejea tena mezaji ," amesema .

Ijumaa Bwana Trump alipandisha juu viwango vya ushuru kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka Uchina zenye thamani ya mamilioni ya dola. Uchina haijatoa kauli yoyote, lakini awali ilitoa wito wa kuwepo kwa "utulivu " katika kutatua mzozo huo wa kibiashara.

Bwana Trump salituma jumbe zenye utata mwishoni mwa juma , kwanza akielezea kusikitishwa na viwango vipya vya ushuru vilivyowekwa na Uchina kwa Marekani, lakini baadae ujumbe huo ukatolewa na White House Jumapili.


Hata hivyo katika kikao cha mataifa yenye utajiri zaidi wa kiviwanda G7 mjini Biarritz Jumatatu alisema kuwa maafisa wa Uchina wamepiga simu mbili "Nzuri , tena nzuri sana " Jumapili usiku na kwamba Beijing ilitaka "kufanya mkataba".

Athari za mzozo wa kibiashara
Jumatatu masoko ya hisa ya Asia yalishuka kuytokana na hofu juu ya vita vya biashara , huku soko la Hong Kong la Hang Seng index likipoteza zaidi ya 3% ya hisa zake kabla ya kuanza kupanda tena baada ya taarifa za kufufuliw akwa mazungumzo.

Hata hivyo hisa katika masoko ya Ulaya zlifanya vizuri baada ya Trump, kutoa ujumbe wa maridhiniano ya kibiashara na Uchina.

Muda mfupi uliopita hisa katika soko la hisa la Ujerumani Dax zilipanda kwa 0.2% huku la Ufaransa Cac 40 likiimarika kwa 0.6% . Katika soko la London FTSE 100 lilifungwa kwa ajili ya siku ya mapumziko ya Bank Jumatatu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad