Moto Waendelea Kuteketeza Msitu Mkubwa wa Amazon

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Bolivia imetoa wito wa kuwepo kwa ushirikiano wa nchi tatu, utakaohusisha Brazil na Paraguay, kuzima moto unaoendelea kuteketeza kwa kasi kubwa msitu mkubwa dunani wa Amazon uliopo kati ya nchi hizo tatu.

Maafisa katika mkoa wa Santa Cruz, wanakadiria kwamba moto huo ulioenea maeneo mbali mbali ya mashariki mwa Bolivia, tayari umekwisha teketeza zaidi ya hekta 450,000.

Aidha, Jeshi la Bolivia linaendelea na juhudi za kuzima moto huo ambao umefikia sehemu ya daraja la Rio Negro, kati ya miji ya Puerto Suarez na Puerto Busch, mpakani mwa Brazil, Paraguay na Bolivia.

Hata hivyo, waziri wa ofisi ya Rais wa Bolivia, Huan Ramon Quintana, ametoa wito wa ushirikiano ili waweze kufanikiwa kuuzima moto huo huku moto huo ukitapakaa na kuendelea kuteketeza msitu huo wa Amazon.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad