AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akimsomea shitaka lake Mwanasheria wa TAKUKURU mkoani Lindi, ameeleza mshitakiwa alikamatwa eneo la Nangando, Liwale Mjini, Julai 28, 2019 majira ya saa 3:00 usiku, akipokea kiasi hicho cha fedha kutoka kwa mlalamikaji ambaye ni mtumishi wa Idara ya Afya.
Mwasheria huyo wa TAKUKURU amedai mahakamani hapo mtuhumiwa aliomba rushwa hiyo kutoka kwa mtumishi wa Afya, ili kumsaidia asichukuliwe hatua za kinidhamu kufuatia uwepo wa malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi.
Ameendelea kusema, kutokana na kitendo hicho mshtakiwa akiwa ni kiongozi wa chama ambacho kinapinga masuala ya rushwa, amefanya kosa kwa mujibu wa kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11/2007.
Hata hivyo mshtakiwa amekana kosa linalomkabili na yupo nje kwa dhamana, na kesi yake imepangwa kusikilizwa tena Mahakamani hapo Agosti 15, 2019.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK