Wasafi Tuwekeni Wazi Mashabiki Kwa Hili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Moja kati ya vitu ambavyo mashabiki tulivipokea kwa furaha sana ni hatua ambayo @diamondplatnumz 

alipoamua kuanzisha lebo ya #WCB lengo kubwa lilikuwa ni kuinua sanaa ya Tanzania na kuwapa nafasi 

vijana wenzake waliopo mtaani. Watanzania tulilipokea kwa mikono miwili na mpaka sasa Wasafi ndiyo 

lebo kubwa ya muziki Afrika Mashariki na kati hili halina ubishi

.

Lakini ndani ya miezi miwili mitatu hii kumekuwa na sintofahamu juu ya kinachoendelea kati ya uongozi 

wa WCB na mtoto wenu wakwanza kimuziki @harmonize_tz Uvumi ni kuwa uongozi na msanii wao hawapo sawa japo kila mtu anajaribu kukwepa kuanika ukweli. Tetesi zaidi zilianza kuvuma baada ya kumkosa @harmonize kwenye 

baadhi ya mikoa inapofanyika tamasha la Wasafi Festival. Inawezekanaje msanii aliyeko chini ya lebo kama Harmonize afanye show moja tu ya Wasafi Fesival?, inamaana uongozi haukuwa na ratiba ya 

msanii mpaka apate mkoa mmoja tu na iko wazi kuwa Harmonize ni miongoni mwa wasanii pendwa 

zaidi kwenye lebo ya WCB?. Mashabiki tunaumia juu ya hili tupo njiapanda

.

Mzazi akikosea hasemwi kwa hali ilivyo sasa mashabiki tunamnyooshea kidole @harmonize_tz kila kukicha. Kinachofuata ni matusi kwenye ukurasa wa Harmonize je kama uongozi mmelitafakari hili?. Msanii anayaoga matusi kila kukicha hamuoni kama mnavunja kitu mlichokijenga 

kwa miaka mingi?, @babutale @sallam_sk @diamondplatnumz mko wapi kutoa maelezo ya kina kwa 

mashabiki?.

.

.

Pia inasemekana kuwa (Taarifa zisizo rasmi) meneja wa Country Boy @petimanwakuache alikutana na maneno makali baada ya kushutumiwa kwamba alitaka kumpandisha Harmonize kama Surprise kwenye tamasha la Wasafi Festival Dodoma. Sasa kwa hali hii tutafika?, WCB mnanguvu kubwa kwenye muziki wa Tanzania na tunawategemea sana sasa kama mnaanza kuvuruga mashabiki wapi tutaelekea?, jitafarini juu ya hili kama ni kiki mnaitengeneza basi jueni hasara zake ni kubwa kuliko faida

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad