Adui wa Chadema, ACT-Wazalendo ni “Nongwa zisizoisha”

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


By Luqman Maloto
Kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2002, vigogo wakubwa wa kilichokuwa chama tawala – Kenya African National Union (Kanu) waligawanyika. Walimsusa Uhuru Kenyatta aliyepigiwa chapuo kugombea urais na Rais aliyekuwa anamaliza muda wake, Daniel Arap Moi.

Majina makubwa kama Raila Odinga, Kalonzo Musyoka, George Saitoti, Joseph Kamotho na wengine walimuasi Moi na kuamua kwenda kupambana na Kanu pamoja na Uhuru wake.

Mwanasiasa kijana, William Ruto alisimama bega kwa bega na Uhuru akimuunga mkono kama mgombea urais wa Kanu kuhakikisha mipango ya Moi inatimizwa.

Upande wa pili akina Raila walikwenda kuanzisha muungano wa National Rainbow Coalition (Narc), ikimjumuisha Kibaki wa Liberal Democratic Party (LDP).

Narc walimsimamisha Kibaki kuwa mgombea urais, kwa hiyo alikwenda kuchuana na Uhuru wa Kanu. Matokeo ya mwisho Kibaki alishinda, hivyo kuhitimisha utawala wa Kanu iliyokaa madarakani kwa miaka 39 tangu uhuru wa nchi hiyo.

Hapo ni kuonyesha kuwa Uhuru na Ruto kama vijana, walishikamana kipindi cha mtikisiko wa Kanu kukimbiwa na vigogo. Wakionyesha uaminifu mkubwa kwenye chama pasipo kumwangusha mzee Moi ambaye aliamini nchi ingekuwa salama zaidi kama angeiacha mikononi mwa Uhuru.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad