AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
JKT Tanzania na Mtibwa Sugar zote zitakutana zikiwa na machungu ya kupoteza pointi sita za mwanzo kwenye ligi ambapo Mtibwa Sugar iliyo chini ya Kocha Mkuu Zuber Katwila ilipoteza mchezo wa kwanza uwanja wa Samora kwa kufungwa mabao 3-1 dhidi ya Lipuli na mchezo wa pili mbele ya Simba uwanja wa Uhuru kwa kufungwa mabao 2-1.
JKT Tanzania chini ya Kocha Mkuu, Abdallah Mohamed ‘Bares’ ilipoteza mchezo wa kwanza mbele ya Simba kwa kufungwa mabao 3-1 na mchezo wa pili ilipoteza ikiwa nyumbani kwa kufungwa bao 1-0 na Lipuli sasa itawakaribisha Mtibwa Sugar.
Bares amesema : ”Tumegundua makosa yetu kwenye michezo iliyopita kwa sasa tunayafanyia kazi mapungufu yetu ili kufanya vema, tunawaomba mashabiki watupe sapoti tunahitaji ushindi hakuna jambo lingine.
Katwila amesema: “Matokeo chanya ndio kitu ambacho tunahitaji, kushindwa kwenye michezo ya nyuuma haina maana kwamba hatuwezi, uwezo upo na makubwa yanakuja, tunahitaji ushindi na inawezekana kwani wachezaji wana morali kubwa.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK