Kalonzo Adai Hamuhitaji Tena Raila 2022

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Nairobi, Kenya. Kiongozi wa Chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka, amesema hahitaji usaidizi wa kiongozi wa ODM, Raila Odinga ili kushinda kiti cha urais kwenye Uchaguzi Mkuu.

Kenya inatarajiwa kuingia katika Uchaguzi Mkuu mwaka mwaka 2022 baada ya Rais Uhuru Kenyatta kuhitimisha miula miwili ya utawala wake.

Musyoka ambaye katika uchaguzi uliopita aliungana na Odinga Raila na kuwa mgombea mwenza alisema tayari ameanza kujitafutia uungwaji mkono wa Wakenya ikiwa ni maandalizi ya uchaguzi huo bila kumtegemea kiongozi huyo.

Alisema aliweka kando azma yake ya kuwania urais mara mbili mfululizo ili kumuunga mkono Odinga na kwamba sasa ni wakati wake kutwaa uongozi.

“Huwezi kuomba uongozi. Uongozi hunyakuliwa,” alisisitiza makamu huyo wa Rais wa zamani aliyekuwa akizungumza katika ibada ya mazishi ya baba wa mwakilishi wa wanawake, Joyce Kamene, mzee David Kasimbi.

Viongozi kadha wa eneo la Ukambani ambako ndiko ngome ya Musyoka wanataka makamu huyo wa Rais wa zamani kumrithi Rais Uhuru Kenyatta atakapostaafu 2022.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad