Mfahamu mtoto wa mkuu wa majeshi Nelson Mabeyo aliyepata ajali ya ndege

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwili wa Nelson Mabeyo ambaye ni mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF), Jenerali Venance Mabeyo unasafirishwa kutoka Serengeti na kupelekwa jijini Dar es Salaam. Nelson akiwa na mwenzake wamefikwa na mauti leo asubuhi Jumatatu.



Serengeti. Helikopta ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) imewasili uwanja wa ndege wa Seronera uliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti nchini Tanzania kwa ajili ya kuuchukua mwili wa Nelson Mabeyo.

Nelson ambaye alikuwa rubani wa ndege ya Kampuni ya Auric air yenye namba 5H-AAM amepata ajali katika uwanja huo akiwa na Nelson Orutu ambaye ni rubani mwanafunzi na wote kwa pamoja wamefariki dunia papo hapo.

Miili ya wawili hao akiwamo wa rubani huyo ambaye ni mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Tanzania (CDF), Jenerali Venance Mabeyo ilihifadhiwa katika Zahanati ya Soronera ikisubiri taratibu zingine.

Helikopta hiyo imetua saa 8.35 ikiwa na watu wanne.


Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdini Babu amesema helikopta hiyo imeelekezwa ichukue mwili mmoja wa mtoto huyo wa Mabeyo na mwili wa Orutu aliyekuwa naye utabaki kusubiri ndege nyingine itakayokwenda Serengeti ikiwa na wataalamu wa masuala ya anga kwa ajili ya uchunguzi wa ajali hiyo.

Chanzo Mwananchi.

By Ally Juma.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad