Kampuni hiyo ambayo katika uzalishaji wa bia hiyo wameshirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Mazingira nchini Sweden imedhamiria kupitia kinywaji hicho kuwashawishi wakazi wa nchi hiyo kuwa ‘Maji taka yaliyotibiwa (recycled sewage water)’ ni maji safi na salama kama yanayotoka kwenye mabomba.
Kwa mujibu wa Taasisi ya Utafiti wa Mazingira nchini Sweden wamesema kuwa changamoto ya watu kutoyaamini majitaka yaliyotibiwa sio ya kiufundi bali ni changamoto ya kisaikolojia na ndio maana wametengeneza bia ili kuwashawishi watu kuyatumia Majitaka yaliyotibiwa.
Kwa sasa PU:REST bia inapatikana pekee katika mgahawa wa New Camegie Brewery’s jijini Stockholm na July 2 itauzwa kwenye migahawa na kwenye matamasha yote nchini Sweden.
______
Usikose Elimu ya pesa ni muhimu mno,na zaidi ukilipia Tsh 1000 ebook hapo Chini unaweza kushinda Tsh Laki moja bofya HAPA