Bondia afariki baada ya kichapo kikali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Bondia Mmarekani Patrick Day amefariki dunia jana Jumatano zikiwa zimepita siku nne tangu atolewe na machela ulingoni baada ya kupigwa na mpinzani wake Charles Conwell katika raundi ya 10 ya pambano lao.

Pambano hilo la Super welterweight lililopigwa Wintrust Arena,Chicago lilikuwa ni la utangulizi kuelekea pambano kuu la uzito wa juu kati ya Oleksandr Usyk na Chazz Witherspoon.

Patrick,27, alipoteza fahamu baada ya kupata majeraha ya ubongo na hivyo kukimbizwa Hospitali huko nchini Marekani ambapo alilazwa mpaka mauti yalipomkuta.

Taarifa iliyotolewa na Promota wake Lou DiBella inasema kuwa, Patrick alifariki akiwa amezungukwa na familia yake, marafiki zake wa karibu na watu wa timu yake ya ngumi.

Wakati Patrick alipokuwa mahututi hospitali, mpinzani wake Mmarekani Charles Conwell,21, aliandika barua ya masikitiko, akisema hakutaka kitu hicho kimtokee Patrick na kueleza kuwa tukio hilo limemfanya afikirie kuachana na mchezo wa ngumi, na pambano hilo linamjia mara kwa mara kichwani kwake na kujiuliza kwa nini tukio hilo limetokea kwani hakuna anayestahili limtokee.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad