Rais Magufuli Awaagiza DC, RPC Kulipa Mil 15 kwa Kumwachia Mwizi – Video

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

RAIS John Magufuli amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa  Rukwa na Mkuu wa Wilaya ya  Nkasi, Said Mtanda,  kuhakikisha wanamlipa mkazi wa Namanyere Sh. milioni 15 ndani ya siku tano kama fidia ya ng’ombe alizoibiwa baada ya mtuhumiwa aliyekiri kufanya wizi huo kukimbia baada ya kupewa dhamana ya polisi.



Mama huyo amemueleza Magufuli kuwa baada ya kuibiwa ng’ombe wake 25 walimkatama mwizi na kumfikisha polisi ambapo alikiri.



“Tulimkamata mwizi tukamfikisha polisi, siku ya pili yake tukalipana Tsh 500,000 kwa kila ng’ombe, hivyo jumla kwa ng’ombe wote 25 alipaswa kulipa Tsh milioni 12.5. Na iliamriwa asiachiwa hadi alipe pesa hizo.



“Lakini tulipokwenda siku ya tatu tukakuta ameachiwa kwa dhamana, sasa hivi ameshakimbia, nimeshafuatilia kwa DC, Takukuru hadi mkoani lakini wamerudishwa ng’ombe wawili tu,” amesema mama huyo.



DC wa Nkasi amesema alishatoa maelekezo kwa jeshi la polisi kumkamata mhalifu na mdhamini na kumfikisha mahakamani.



Aidha Rais Magufuli amesema:

“Kwa sababu hamkuchukua hatua mapema, wewe DC na RPC nawapa siku tano mmulipe huyu mama shilingi milioni 15 na za usumbufu. Kazi ya polisi mkikamata mhalifu ni kumfikisha mahakamani, wewe DC ndiye Mkuu wa Ulinzi na Usalama wa Wilaya, kama jambo lilikuwa gumu ungemtarifu Mkuu wa Mkoa au ungenipigia mimi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad