RC Makonda Atangaza Neema Ya JPM Kigamboni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amemshukuru Rais Dk John Magufuli ‘JPM’ kwa kutoa kiasi cha shilingi bilioni 90 za ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kwenye Wilaya ya Kigamboni.



Barabara hiyo inaanzia Kibada kuzunguka Mwasonga na Kisarawe Two ikiwa ni sehemu ya kutatua kero za ubovu wa barabara kwa wananchi wa wilaya hiyo.



Makonda ameeleza hayo leo wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo wilayani Kigamboni na kueleza kuwa Serikali imedhamiria kufanya Mji wa Kigamboni kuwa wa kisasa.


Katika ziara hiyo, Makonda ametembelea ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni lenye thamani ya shilingi bilioni 5.3 ambapo amewataka TBA kuhakikisha wanakamilisha jengo hilo kabla ya Desemba 30 na kubainisha kuwa jengo hilo ndilo jengo kubwa kuliko majengo yote ya halmshauri hapa nchini.


Aidha, Makonda ametembelea ujenzi wa Majengo 7 ya Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni ambayo ujenzi wake umekamilika na kugharimu shilingi bilioni 1.5 hivyo kupongeza manispaa hiyo kwa kukamilisha ujenzi huo mapema.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad