AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa ya bodi ya madaktari wa timu ya Taifa ya Misri imethibitisha kuwa mchezaji wa Liverpool, Mohamed Salah mwenye miaka 27 hali yake haipo sawa.
Salah ana maumivu ya ‘enka’ ambayo aliyapata kwenye mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza dhidi ya Crystal Palace hali iliyomlazimu aukose mchezo dhidi ya Manchester United.
Kiongozi wao Dr.Mohamed Abul-Ela amethibitisha kwamba bado Salah hajawa tayari kucheza mechi za ushindani kwa sasa.
“Mchezaji alikuja kambini Jumanne jioni akawa chini ya uangalizi hata alipokuwa akifanya mazoezi uwanja wa Burj Al Arab alikuwa kwenye uangalizi,” ilieleza taarifa hiyo.
Salah atakosa mchezo dhidi ya Kenya na Comoro ambayo ni maalumu kwa ajili ya michuano ya Afcon kwa kuwa anahitaji muda mrefu kurejea kwenye ubora.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK