AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Ulega amesema hayo wakati akijibu swali bungeni leo wakati akijibu Swali lililoulizwa na Mbunge wa Jang’ombe, Ali Hassan King aliyetaka kujua gesi ina madhara gani katika uvuvi wa kuzamia.
“Kwenye kina kirefu cha maji inawezekana nyavu ikakwama kule chini hivyo mvuvi anaweza akatumia gesi kuzamia na kitu kingine kwa baharini maji yanaweza yakakifika hata kwa miguu lakini haja ya gesi inakuwepo pale maji yanapojaa sasa chupa inaharibu kitu gani kwasababu mabomu yanaweza yakategwa bila hata ya chupa,” amehoji.
Akijibu swali hilo Ulega amesema utafiti walioufanya umebainisha kuwa wavuvi wanaofanya uzamiaji wengi wao wanaambatana na shuguli za uvuvi haramu ndiyo maana serikali ikasema itazuia zoezi hilo isipokuwa kwa wale wenye kibali maalumu.
“Ugomvi wetu siyo chupa bali ni matumizi yanayotokana na matumizi ya gesi, tunafahamu katika bahari umbali kwa maana ya kina kilomita 40 mvuvi ni lazima atafute namna ya kumfanikisha kufanya shughuli yake lakini kwa utafiti wetu hapo nyuma ilionekana wazi kwamba waliokuwa wanafanya uzamiaji walikuwa wanaambatana na shuguli za uvuvi haramu ndio maana serikali ikasema itazuia zoezi hilo isipokuwa kwa wale wenye kibali maalum.
“Wavuvi haramu wanaotumia milipuko hutumia mitungi ya gesi kuzamia kwaajili ya kukusanya samaki waliowaua kutokana na milipuko hiyo, athari za milipuko ni pamoja na kuharibu matumbawe na mazingira ya baharini kwenye maji ambayo ni mazalia na makulia ya samaki pamoja na viumbe wengine na hivyo kuhatarisha uendelevu wa rasilimali za uvuvi nchini,” amesema Ulega.
Ameongeza kuwa kwa sasa serikali iko katika kuboresha sheria na kanuni za uvuvi na kwamba wamesikia kilio cha wavuvi wazamiaji na hivyo wanakifanyia kazi endepo sheria hizo zitapitishwa na wanaamini katika mambo yatakayoenda kuboreshwa hilo ni mojawapo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK