Wapangaji wa Nyumba za NHC Kuhakikiwa Upya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Waziri wa Ardhi Mhe.William Lukuvi ametoa miezi 4 NHC kuhakiki wapangaji wa nyumba pamoja na majengo yao na kisha kuanzisha nyaraka za Kielektroniki zitakazosaidia kubaini wajanja wanaopangisha na kujimilikisha nyumba za shirika hilo kinyume cha sheria.

Lukuvi, alitoa agizo hilo jana jijini Dar es Salaam baada ya juzi kutembelea miradi ya shirika na kutaka ifikapo Machi 30, mwakani, uhakiki huo uwe umekamilika.

“Ninajua kuna baadhi ya wapangaji wameanzisha vishirika vya nyumba ndani yenu, kuna watu wana nyumba mbili au tatu kwa ujanja wao na wao wanakodisha. Tutawaondoa wapangaji hewa na tutawatambua wamiliki hewa wa nyumba zilizotaifishwa.

“Kuna watu wakihama kwenye nyumba wanaziuza kwa gharama kubwa wanachukua fedha juu ya mgongo wa shirika hili kwa sababu inaelekea hatuna utunzaji wa kisasa wa takwimu za wapangaji na nyumba.”

Pia, alilitaka shirika hilo liingie kwenye utaratibu wa kidijitali kwa kuanzisha nyaraka za kieletroniki ili kutunza kumbukumbu za wapangaji.

“Taarifa hizi ziingie kwenye mfumo wa Mamlaka ya Vitambulisho Vya Taifa (Nida), wapangaji wote lazima wafanyiwe uhakiki taarifa zao zifanane na taarifa za Nida.

“Kila mpangaji anapohamia kwenye nyumba tumjue anafanya kazi wapi, jina lake kamili kama alivyojiandikisha Nida.”

Alisema anawajua baadhi ya watu wanaomiliki zaidi ya nyumba moja kwa majina tofauti na wengine wanazitumia kuzikodisha huku wakiwa kwenye majengo mengine.

“Wote watambuliwe, najua kuna vishoka ambao wanaowatumia kuzikodisha, mfanye uhakiki upya wa kielektroniki. Wakati wa uhakiki hakikisheni maofisa na mameneja wa Mkoa wa Dar es Salaam wanaondolewa na kuwekwa watu wengine,” alisema.

Waziri Lukuvi aliwaeleza wananchi kuwa nyumba za shirika hazitolewi kwa familia kama urithi baada ya aliyepangishwa kufariki, bali waliobaki hutakiwa kwenda NHC kwa ajili ya upangaji upya.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad