AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Jeshi la Polisi mkoani Katavi, linamshikilia mganga mfawidhi wa kituo cha Afya Inyonga wilayani mpanda, Calvin Mnaso (37) kwa tuhuma za kuiba dawa za binadamu pamoja na vifaa tiba katika kituo hicho.
Kamanda wa polisi mkoa wa Katavi, Benjamin Kuzaga ametoa taarifa jana kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Desemba 19, baada ya polisi kupata taarifa za wizi katika kituo hicho.
Amesema baada ya taarifa hizo jeshi la polisi walianza kupekua katika nyumba za baadhi ya watu waliohisiwa kuhusika na wizi huo wakiwemo baadhi ya watumishi wa kituo hicho cha afya.
Kamanda Kuzaga amesema walipofika nyumbani kwa mtuhumiwa na kufanya upekuzi walifanikiwa kukamata mabox matano ya dawa mbalimbali za binadamu, vifaa vya kupima maradhi ya binadamu, vifaa vya kufanyia oparesheni na tohara, godoro moja pamoja na sindano ambavyo vyote ni mali ya serikali.
Hadi sasa mtuhumiwa huyo bado anashikiliwa na polisi na upelelezi ukikamilika anatarajiwa kufikishwa Mahakamani kwa mujibu wa sheria.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK