Mzimu wa Balaa Kwa Makocha Waikumba MBEYA City...Juma Mwambusi Ajivua Gamba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kocha Juma Mwambusi ameandika barua ya kujiuzuru kuifundisha timu Mbeya City, kutokana na mwenendo mbovu wa matokeo kwenye michezo ya ligi kuu ya soka Tanzania bara msimu huu.

Kikao cha Bodi ya Mbeya City FC kilichofanyika leo Jumamosi kwa pamoja kimeridhia ombi la kocha huyo kujiuzuru.

Taarifa hiyo ilieleza kwamba Mwambusi aliwasilisha ombi la kujiuzuru tangu Novemba 26 mwaka huu kwa maslahi mapana ya klabu kufutuatia mwenendo usioridhisha wa timu tangu kuanza.


“Katika kipindi hiki cha mpito Bodi yetu imemkabidhi timu Kocha Msaidizi Mohamed Kijuso huku mchakato wa kumtafuta kocha mkuu ukiendelea” ilisema taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, James Kasusura.


Taarifa hiyo ilieleza zaidi kwamba Bodi inamshukuru Mwambusi kwa mchango wake mkubwa kwa maendeleo ya timu na bado inahitjai ushauri na uzoefu wake katika tasnia ya michezo.

Mbeya City inashika nafasi ya 18 ikiwa na pointi nane katika michezo 12 waliyocheza.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad