AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema ndege za kijeshi za Israel zimetumia ndege ya abiria kama ngao ya kujikinga katika uvamizi wake mpya dhidi ya Syria.
Msemaji wa wizara hiyo, Meja Jenerali Igor Konashenkov alisema jana Ijumaa kuwa, ndege ya abiria ya Airbus-320 iliyokuwa na abiria 172 nusra ipigwe na makombora ya mfumo wa Kujikinga ya Syria kielekea Damascus kutoka Tehran wakati ndege za Kijeshi za Israel zilipofanya mashambulizi.
Hata hivyo mfumo wa ngao ya makombora ya Syria mjini Damascus ulifanikiwa kutungua makombora hayo ya Israel.
Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi ameeleza bayana kuwa, baada ya kukoswakoswa na makombora , ndege hiyo ya abiria ililazimika kutua kwa dharura katika uwanja wa kijeshi wa Hmeymim katika mkoa wa pwani wa Latakia, magharibi mwa Syria.
Meja Jenerali Konashenkov amekosoa mienendo hiyo ya Israel ya kufanya mashambulizi yake ya makombora bila kujali ndege za abiria zinazoruka katika anga ya Syria
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK