"Godbless Lema Amezungukwa na Polisi Hotelini" - Makene

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa Polisi wamezunguka hoteli aliyofikia Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema, huku wakishinikiza uongozi wa hoteli hiyo kuwaonesha chumba alicholala Mbunge huyo.

Akizungumza na EATV&EA Radio Digital leo Machi 17, 2020, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho Tumaini Makene, amedai kuwa mpaka sasa hawajajua sababu ya polisi hao kujazana hotelini hapo.

"Lema amezungukwa na Polisi Hotel ya Regency Park, Polisi wamefika pale tangu asubuhi wanamtafuta na sababu haijajulikana na wana silaha, wamelazimisha wapelekwe chumba alicholala na uongozi wa hotel umekataa maana siyo utaratibu, kwahiyo hadi sasa wako hapo wanamngoja" amesema Makene.

Mbunge Lema leo ilikuwa afanye mkutano na waandishi wa habari, kujibu madai ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) dhidi yake.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad