Mama Mwenye Nyumba Anataka Kuniozesha Mwanae Kinguvu Nguvu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Husika na kichwa cha habari hapo juu,

Mimi ni mpangaji nimepanga nyumba moja hapa mjini na nina kama miezi sita kwenye hii nyumba niliyopanga ambayo mpangaji ni mimi mwenyewe mama mwenye nyumba ni mjane yaani single mother na ana watoto watatu wote wa kike.

Kinachonisukuma kuomba ushauri hapa ni nyenendo za huyu mama na binti yake mmoja yule wa pili, yaani huyu mama anaforce mwanae nimuoe yaani niishi nae gheto kwangu niwe nalala naye na kuamka naye.

Kila chakula kikiiva naletewa nguo nafuliwa na hadi maji bafuni napelekewa na wanafanya yote haya si kwamba mimi nataka hapana ni kwa lazima, yaani chakula unaletewa ki nguvu nguvu kama ni wali unakuwa hadi ushamwagiliziwa maharage na mchuzi sasa kwa mazingira haya ni vigumu sana kukataa.

Jana binti kaja usiku kuniletea msosi na hakurudi tena ndani kwao akabaki hadi asubuhi, mimi leo nimeondoka kwenda kazini nimemuacha gheto nimerudi nimekuta kapika chakula chetu wawili tofauti na chao kile cha kwa mama yake.

Sasa kwa staili hii ya kuja gheto Jana usiku na leo nimemkuta kapika si tiari nishakabiziwa mzigo hivi.

Ushauri wenu nifanyaje? Nihame hii nyumba au nifanye nin?


LONDON BABY
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Unavyooa inabidi uoe ukiwa tayari umeshapanga, umempata yule unayempenda kwa dhati na mnapendana, unamjua tabia zake na anakujua tabia zako.Kamwe usioe mwanamke kwa kumuonea huruma, kulazimishwa. Ni kosa kubwa sana ambalo litakugharimu maishani siku zijazo. Nakushauri uhame haraka sana hapo. Ndoa hailazimishwi mheshimiwa.

    ReplyDelete

Top Post Ad