AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mkuu wa idara ya habari na mawasilino ya klabu ya Simba Haji Sunday Ramadhan Manara amesema masuala yanayohusu uwekezaji kwenye klabu hiyo yanawahusu Wanachama na Mashabiki wa Simba.
Siku za karibuni baadhi ya vyombo vya habari hasa redio zimekuwa zikiendesha vipindi vya mijadala ambapo moja ya mijadala hiyo ilihoji hatma ya Bilioni 20 ambazo mwekezaji wa klabu ya Simba Bilionea Mohammed Dewji ‘Mo’ aliahidi kuziweka kwenye akaunti ya mabingwa hao wa nchi baada ya mchakato mzima wa uwekezaji kukamilika.
Manara amesema kimsingi wapenzi, wanachama na mashabiki wa Simba ndio wenye uhalali wa kuhoji masuala yanayoihusu klabu yao na sio kila mtu afanye hivyo kwa utashi wake.
“Wenye uhalali wa kuhoji kuhusu Bilioni 20 za mwekezaji wa Simba ni mashabiki wenyewe ambao walimpa timu, siyo mtu mwingine tu ambaye hana uhalali,” amesema Manara
Mo alishinda zabuni ya uwekezaji kunako klabu ya Simba mwaka 2017 akinunua hisa asilimia 49 kwa kiasi hicho cha fedha.
Tangu wakati huo Mo amekuwa ndiye msimamizi mkuu wa klabu ya Simba akilipa mishahara ya wachezaji pamoja na kununua wachezaji wapya.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK