Mambo Ambayo Wanawake Wanafanya ili Kuleta Mvuto Lakini Hayashtukiwi na Wanaume Kivile

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

1. Kubadili mtindo wa kujikwatua.

Mwanamke anaweza kuwa amezoea kujikwatua kwa namna fulani lakini baada ya muda akaamua kubadili muonekanao wake kwa kubadilisha aina mpya ya kujikwatua kwa kuongeza vikorombwezo fulani fulani akitegemea mwenzi wake ata notes lakini asijue kwamba wanaume kwenye jambo hilo wala haliwagusi kabisa mpaka wafanye kushtuliwa.

Kwa hiyo nawashauri tu msije mkaumia bure pale mnapoona wenzi wenu hawa notice mabadiliko mliyoyafanya ndivyo tulivyo....

2. Kubadili mtindo wa nywele.

Kwa kawaida wanawake hutumia muda wao mwingi kutengeneza nywele zao ili kujipa mwonekano mpya na pia wakitarajia kwamba wenzi wao watapenda, lakini cha kushangaza wenzi wao wala haiwagusi na wala hawa notice mabadiliko hayo ya nywele mpaka wafanye kushtuliwa na wenzi wao. jambo hilo huwa linawakwaza sana wanawake, lakini labda tu niwape ushauri wa bure, msiweke matarajio makubwa ya kudhani kwamba mabadiliko ya nywele mnayoyafanya yatawavutia wenzi wenu, si kweli utafadhaika bure bora tu mfanye kwa utashi wenu 

3. Kubadili rangi za kucha

Wanaume wengi hawajui tofauti ya rangi, kwa hiyo hata mwanamke abadili rangi yake ya kucha kwa ajili ya ku match na mavazi fulani aliyonunuliwa na mwenzi wake au hata aliyonunua mwenyewe anaweza kushangaa mwenzi wake asishtukie jambo hilo. Ajabu eh!

4. Mkoba mpya.

Unaweza kukuta mwanamke kajinasibu na kununua mkoba mpya wa gharama baada ya kujinyima sana akitegemea mwenzi wake atauona na kumsifia lakini atashangaa mwenzi wake wala haulizi anaona tu kama ni mkoba wa kawaida. Lakini pia hata kama mkoba wenyewe ume match na mavazi bado ni ngumu kwa mwanaume ku notice na ndiyo maana inawauma sana wanawake wengi. Mtuhurumie tu, ndivyo tulivyo....
5. Kiatu kipya

Viatu navyo ni eneo lingine ambalo wanaume hawa notice kabisa, mwanamke anaweza kununua kiatu kipya akitarajia mwenzi wake atakiona na kumsifia lakini wala, labda tu kama mwanaume huyo anapenda aina hiyo ya kiatu na aliwahi kukisifia baada ya kumuona mwanamke mwingine amekivaa na kikampendeza, lakini kama si mpenzi wa viatu wala mwanamke asitarajie kusifiwa, ni mpaka pale atakapomshtua mwenzi wake kwa kumuuliza kama kiatu alichovaa kimempendeza au la na sije akashangaa akijibiwa kwa kifupi tu, "ndiyo" bila comments.
Kwa kawaida wanawake wanapenda ukiwasifia kuhusu jambo fulani utoe na comments japo kidogo tena kwa undani kabisa....

6. Lebasi za ulimbwende na makochokocho mengine

Hereni, bangili na kishaufu au kipini cha puani kinaweza kumpa mwanamke muonekano mpya, lakini muonekano huo hauwezi kumshangaza mwanaume kama mwanamke anavyotarajia, jambo hilo huwa linawakera sana wanawake lakini ukweli ndiyo huo wanaume hawasumbuliwi na vitu vidogo vidogo. 
7. Pambo jipya chumbani au kitandani

Mwanamke anaweza kubadili mwonekano wa nyumba au wa chumba cha kulala akidhani kwamba jambo hilo litamvutia mwenzi wake. si kweli wanaume hawako hivyo anaweza akafika nyumbani na kuona kama vile hakuna kilichofanyika mpaka afanye kushtuliwa na mwenzi wake kwa kuulizwa kama ameionaje nyumba au chumba chao cha kulala. haishangazi mwanaume akiuliza kwani kuna nini....!

Kwa mwanamke jibu hili anaweza hata kutamani kumtwanga mwanaume na flower verse kwa hasira, lakini mianaume ndivyo tulivyo, mtuhurumie tu.


----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mimi huwa nagundua mapema na kusifia ikiwa mke wangu atabadili mapishi na menu jikoni lakini kubadili badili say mtindo wa nywele naona kama anajihangaisha tu bure.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kabisa havina kitu hivyo kikubwa ni ukarimu,umakini,hekima,usafi na kufanya mambo sahihi kwa nyakati

      Delete

Top Post Ad