Mbinu Za Kumfanya Mwanamke Akupende na Kukuzawadia Tunda Bila Hata ya Kumtongoza

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Wanawake wengi huwa hawajui ni kitu gani kinachowafanya wanase kwenye mitego ya wanaume. Hawajui kuwa wanaume wengi hutumia hizi njia kuwafanya wanawake wawapende kila siku. Hizi ndizo njia za kuwanasa.

Wanaume wengi hushangaa na kujiuliza, kwanini wanawake wengi huvutiwa na wanaume wengine, lakini sio wao.

Je wanatatizo au mapungufu fulani? Ni kitu gani wanakikosa ambacho hao wengine wanacho/ wanavyo?

Usijali, katika huu mchezo wa kuwavutia wanawake, haikuhitaji uwe na fedha nyingi kwenye account ya benki, au uwe na gari zuri sana kuliko wanaume wote ndo uwavutie wanawake – kinachowavutia ni mwanaume anaye

jua na anayeweza kuwavutia

Jinsi gani ya kumvutia mwanamke na akupende bila ya wewe kumwambia

#1 Usioneshe unampenda sana. Kwa muda mrefu, kumekuwa na utamaduni wa mwanaume kumwonesha mwanamke anampenda sana ili aweze kukubaliwa, na wanawake ndo wamejijengea utamaduni wa kufatwa. Hii inawapa wanawake uhuru wa kuchagua mwanaume wanayemtaka na kuwatema wasio wataka.

Japo, unaweza ukageuza mambo kwa kuwa karibu na mwanamke na kumfanya yeye ajue kwambw awewe haumuhitaji yeye au hauna lengo la kumtongoza au kumtaka, kwa maana hiyo huna haja ya kumuomba kitu yeye akukubalie. Punguza hisia, zisikuendeshe ssana hatakama unamuhitaji. Hii itamfanya mwanamke akuone wa tofauti kwa sababu wegi wanamsumbua lakini wewe haumsumbui, hivyo atajitahidi afanye kila linalowezekana ili akuvutie(Hivyo umegeuza kibao)

#2 Wakati mwingine KATAA. Usiwe mwepesi wa kukubaliana na kila jambo, wanaume wengi ili wakubaliwe huwa radhi kufanya lolote wanaloambiwa hatakama hana uwezo ili tu amvutie mwanamke. Kama kweli unataka kumvutia mwanamke , hautakiwi kuanguka kwenye huu mtego. Usimvutie kiti ili akae, usimnunulie kinywaji, muda mwingine puuza maombi yake, na ikiezekana kwa baadhi ya mambo useme “HAPANA”.

#3 Usiwe rafiki sana. Jijue kuwa wewe ni mtanashati na mwanume halisi. Kama unaingia bar au mgahawani na huyu mwanamke anakuangalia tangu unaingia , nenda kakae kwenye kiti kilichopo karibu na yeye – ikiwezekana umtazame. Hapo mawazo yake yatakuwa yashampeleka kwamba unataka kumuagizia kitu eidha kinywaji au chakula.

Badala yake, achana naye na sura yako bila kujtabatamisha sana agiza kinywaji chako mwenyewe na usimwangalie tena, fata yako. Haya mambo yatampagawisha na itamfanya yeye sasa, afanye jambo lolote ili aweze kukuvutia.

#4 Mfanye awe na wivu. Njia nyingine ya kumfanya mwanamke akupende bila ya kumwambia, ni kuzitumia hisia zake kumuangamiza mwenyewe. Kama unajua anakutamani / kukupenda, mfano, jaribu kuonesha kuwa unatoka na mwanamke mwingine. Kama ni rafiki yako, mwambie kabisa unataka umfanyie vitu vya makusudi vitakavyo mtamanisha mwanamke mwingine. Kwa kumfanya huyo mwanamke awe na wivu, unacheza na hisia zake. Atafanya kila analoweza ili umpende yeye na umuone yule mwanamke uliyenaye siyo kitu.[Soma:Ishara 12 zinazoashiria kabisa anakutaka wewe na anataka umuombe kutoka out!.]

#5 Mchanganyie ishara. Wakati mwingine mwangalie kabisa – macho – masikio – pua vimuelekee yeye. Kama unaongea naye jifanye kama unamsogelea taratibu, kumtamanisha alafu gafla rudi nyuma na uegemee kiti chako. Au, Mwambie yeye ni mwanamke mzuri ana alafu wakati huo umwangalie mwanamke mwingine anayepita pembeni.Haya mmbo yatamchanganya. Hii itamfanya yeye ahisi kuwa anahitaji kufanya vitu vingi zaidi ili aweze kukuteka.

#6 Usitabirike. Kuwa wa tofauti na wanaume wengine ambao alishawahi kuwaona. Fanya kitu kitakaho mfanya asipate picha halisi ya ni nini unamaanisha. Wanawake wengi sana hukerwa na wanaume wanaotumia style moja kuwafata au kufanya mambo kwao. Muahidi utampigia simu muda fulani lakini ukifika ule muda, usimpiigie subiri saa kadhaa zipite ndo umpigie. Utamfanya yeye atamani kusikia neno lolote kutoka kwako lakini hatalipata kwa muda huo. Kwa namna hiyo atakuwa anafikiria sana kuhusu wewe kwa wakati huo.

#7 Uwe mwepesi. Hii ni njia nyingine ya kumfanya mwanamke akupende – kuwa mwepesi wa kufanya mambo ya akili. Jifanye kuwa wewe ni zaidi yake. Vaa vizuri na usiogope kuonesha vitu vizuri ulivyonavyo. Iwe kazini, au mtaani, kama ushajua anachokipenda kuona kutoka kwako – kitumie hicho kitu. Kama kasema anaipenda movie fulani, mwambie jinsi hiyo movie usivoipenda hatakama haumaanishi.

#8 Mfanye ajisikie mpweke. Kuwa mwema na mkarimu na mchangamfu kwa kila mtu – isipokuwa yeye. Hii itamfanya ajistukie – na aone kama vile yeye kuna kitu amepungukiwa au kujiuliza yeye anatatizo gani. Hata penda hivyo. Kwa hiyo atajitahidi kwa namna yeyote anayoweza kufanya mambo yatatamani uwepo wako – au uyaelewe mambo yake anayofanya.

#9 Mwambie mapungufu yake. Wanawake wengi huwa makini sana katika mambo wanajua ni mapungufu kwao, mfano uzito wao, syle ya maisha, lugha, kwa kuorodhesha vichache. Kama unataka mwanamke akupende muda wote, mfanye ajione hajakamilika.

Mfute kidogo kwenye shavu lake hatakama hana uchafu, mwambie leo hajapendeza – au makeup imemuharibu, au mwambie kuwa unahisi kaongezeka uzito au kanenepa kiasi cha kutisha, hatakama hajanenepa kweli.

#10 Msifie. Njia nyingine ya kumdatisha mwanamke ni kumsifia. Wakati unavoweza kumponda – vivyo hivyo msifie pale anapostahili. Mwambie nanavyonukia vizuri – au nywele zake alivyopendeza, na utamfanya moyo wake uende kasi.

#11 Mfanye ajistukie. Muda mwingine mwambie ni katoto au kituko au wakutamaniwa. Mwambie vyovyote vile vitakavyomfanya abaki na maswali. Hii itamfanya muda wote akuwaze na awe anatilia maanani kila unachomwambia. Mfano, kama utamuuliza aliwaza ini kuhusu njia A ya kukusanya mapato ya biashara, akasema ameshaitumia tayari na ameongeza mapato kwa 19%, mwambie, “Nilijua, utakuwa unatumia mifumo midogo kama hiyo . Sasa, hii ni njia B niliyoiona itakusaidia kuongeza mapato kwa 50%…”

#12 Mkatishe. Muanzishie maongezi, na muulize kitu ambacho unajua anakipenda sana kukiongelea. Na wakati ndo anataka aikoleze story yake, mkatishe na mwambie, “Ohhh.. samahani nilisahau, natakiwa kukutana na mtu muda sio mrefu. Bye!”

Na bila kusita, ondoka na umuache mwenyewe. Hii itamuacha kachanganyikiwa, kwasababu alikua bado hajamalizia story yake. Hapo sasa utakuwa na ujiko wa kumtafuta siku nyingine ya kumuomba mtoke wote ili akakumalizie story.

#13 Mfanye ajione akakimbele mbele sana. Wakati ulimwengu wa mapenzi ukiendelea kubadilika kutokana na utandawazi, sheria za kimapenzi nazo pia zinabadilika – lakini bado wanawake wana udhaifu katika mapenzi. Kwa hiyo muda mwingine mwanamke akikufata – mwambie, “..Unajaribu kunitega au? Kwa sababu kama unalengo hilo, Mimi sipo huko kabisa”.

#14 Kuwa mtawala. Simaanishi umuendeshe kwa kila jambo – Hapana. Kuwa muwazi kwa kile unachokitaka katika mahusiano yenu. Kwa lugha nyingine usifiche makucha, hii itamdhihirishia kuwa sio muda wote utakuwa unafata kile anachokitaka. Mfanye ajue mwanzoni kabisa kuwa wewe ni mtu wa aina gani na maisha yako yakoje ukiwa single, jinsi unavyo ishi kwa furaha ukiwa mwenyewe, kwa maanai hiyo hautaki kuingia kwenye mahusiano ambayo yatakuwa yanakupa msongo wa mawazo(stress).Muoneshe ni jinsi gani upo tayari kuwa mwenyewe kuliko kuwa na mtu anayekuendesha. Hii itamsaidia yeye ajue asimame wapi na ni vitu gani inampasa asivifanye.

#15 Jifunze mchezo mchafu wa kutongoza. Mfanyie kitu kimoja kitakachomfanya akupende sana, kisha baada ya hapo muache

#16 Mpe story za uongo. Wanawake hupenda sana maigizo. Huwa na huzuni kwa story zihuzunishazo alafu baadae hufurahi. Kwa hiyo kabla haujamfata mwanamke, fikiria kitu au jambo lililokugusa kimaisha la kuhuzunisha sana. Ongeza vichumvi kidogo ili story iwe tamu utakapoanza kumsilmulia. Kitu cha muhimu hapa ni kuleta furaha na uzuni = = igizo, na hapo atakuwa anakuangalia kwa huruma kama katoto ka mbwa kanachohitaji kupewa chakula.

#17 Kuwa msiri. Ukikutana na mwanamke yeyote yule, usije ukampa taarifa zako zote zinazokuhusu wewe kirahisi hivyo. Kama kakuuliza kuhusu kazi yako na wewe ni fundi ujenzi, mwambie, ninatengeneza tengeneza vitu hapa na pale, na ishia hapo. Kwa kufanya hivyo utamfanya awe anawaza, na kukuwaza wewe zaidi.

#18 Baada ya hapo, tumia silaha yako ya siri(secret weapon). Lile neno “L”. Hakuna neno linalowamalizaga wanawake nguvu kama neno “I Love You – Nakupenda”. Kama mtakuwa mmeshazoeana na wakati mwingine huwa mnatoka out, usiogope kumwambie kuwa unampenda, na umwambie hili katika hali ya juu kihisia na wakati wote mpo katika hali kubwa ya utulivu. Ukiupatia muda wa kumwambia, hakuna kitakachomfanuya akatae.

#19 Mshike. Hii ni njia nyingine ya kumtamanisha bila hata ya mumwambia neno lolote. We mshike tu. Kama ni rafiki yako sana au kwa kiasi fulani, mshike mkono wake – kama vile haukutarajia, na hapo lazima umdake.

Au kama tayari mmeshazoeana na huwa mnatoka out, unaweza mshika mabega au mashavu. Hii itapeleka signal kwenye mwili wake, na ataanza kujenga hisia na matarajio ya wewe kumwambia kitu – na hicho ndicho ulichokuwa ukikitaka.

#20 Jiamini. Dhihirisha kwamba unaweza kuishi bila yeye. Mvuvi anapokwenda baharini anakuwa anatafuta samaki, akimkosa / akiwakosa sehemu moja haimaanishi ndo mwisho wa maisha yake – hii inampa muda wa kuingia ndani ya bahari zaidi ili kupata samaki wengine. Mfanye ajue kuwa yeye siye mwanamke pekee duniani hatakama unampenda.

OPEN IN BROWSERCOMMENTS
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad