Runinga ya Kenya yajuta kumuita rais Magufuli 'Mkaidi'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Runinga yenye watazamaji wengi nchini Kenya imesema katika taarifa iliotangazwa katika chumba hicho cha habari kwamba inajuta kumuita rais Magufuli 'mkaidi' , katika ripoti yake iliozungumzia kuhusu sera zake katika kukabiliana na mlipuko wa virusi vya corona.

Tanzania haijaweka masharti makali kuhusu mikutano ya watu kama ilivyofanywa na mataifa mengine duniani.

Katika ripoti hiyo ya runinga ya Citizen iliopeperushwa hewani tarehe 22 mwezi Machi , bwana Magufuli alinukuliwa akisema kwamba mlipuko wa virusi vya Covid-19 haufai kutumiwa kama sababu ya kuathiri uchumi wa Tanzania.

Runinga hiyo inayopeperusha matangazo yake katika eneo la Afrika Mashariki , ilisema katika ripoti hiyo kwamba haikuwa na madhumuni ya kuwapotosha raia wa Tanzania.

Taarifa hiyo ilisema :
Tunanukuu: Tarehe 22 Machi , tuliripoti kuhusu mipango iliowekwa na serikali ya Tanzania kukabiliana na janga la virusi vya corona. Katika ripoti hiyo tulimuita rais Magufuli 'mkaidi'.

Tunanukuu ujumbe: Katika mahojiano na runinga ya Citizen , balozi wa Tanzania nchini Kenya alisema kwamba Magufuli anaunga mkono juhudi za kieneo na kimataifa kukabiliana na mlipuko wa virusi vya corona .

Tunanukuu ujumbe: Utumizi wa neno 'mkaidi' dhidi ya rais Magufuli hauna msingi .

Idadi ya wagonjwa Tanzania yafikia 88 baada ya wengine 29 kuthibitishwa
Serikali ya Tanzania ilithibitisha wagonjwa 29 wapya wa virusi vya corona siku ya Jumatano .

Kulingana na taarifa ya wizara ya Afya nchini humo wagonjwa 26 kati yao wapo katika mji wa Dar es Salaam huko wawili wakipatikana mjini Mwanza na mmoja akiwa katika eneo la Kilimanjaro.

Waziri wa Afya Ummi Mwalimu alisema kwamba ufuatilianaji wa watu waliokaribiana na wagonjwa hao unaendelea.

Hatahivyo waziri huyo alitangaza habari njema akisema kwamba hadi kufikia Jumatano takriban watu 11 wamepona virusi hivyo lakini akaongezea kwamba watu wanne walifariki.

Ongezeko hilo la wagonjwa linajumlisha wagonjwa wapya sita waliotangazwa na waziri wa Afya wa kisiwa cha Zanzibar.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. DR,MDIRO KAMA WAHITAJI PESA ZA MAJINI,DAWA YA MAPENZI, NDOA, KUMVUTA UMPENDAE, MIGUU KUWAKA MOTO, KULINDA BIASHARA NA DAWA YA MAPENZI, JE UNAMATATIZO, KARIBU KWA KUFATA MASHARTI NA KUTIMIZA UTAFANIKIWA
    (MALIPO YA NDAGU ZA MALI AU MAJINI NI BAADA YA MAFANIKIO)
    (KWANINI USUMBUKE)
    NAITWA DR, MDIRO piga 0742162843. KAMA UNAITAJI PESA ZA MAJINI AU NDAGU YA MALI AU UTAJIRI NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU), NDOA, MIKOSI, MABALAA, JINI MAHABA NA SHIDA YA UZAZI. NIPIGIE 0742162843. KIKUBWA NI KUSIKILIZA NA KUFATA MASHARTI. ANGALIZO USITUME SMS PIGA NA UWE NA NIA.

    (kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
    1. uwe una umri wa miaka 18+
    2. uwe tayari kupokea masharti yote
    3.uwe na uwezo wa kutunza siri
    4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote 
    PIGA SIMU KWANZA HUSITUME SMS

    ReplyDelete

Top Post Ad