Mtendaji Atiwa Mbaroni Kisa Kupapasa Matiti ya Mtoto wa Miaka 14

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mtendaji wa Mtaa wa Kyakailabwa Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba akikabiliwa na mashtaka mawili ya kumtorosha mtoto mwenye umri wa miaka 14 na kumfanyia shambulio la aibu la kumpapasa matiti.


Kesi hiyo namba 149 ya mwaka 2020, imesomwa Mahakamani hapo na Wakili wa Serikali Joseph Mwakasege, mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo Ruth Migan, amesema mshtakiwa huyo Patrick Rwegasira mwenye umri wa miaka 44 baada ya kumtorosha mtoto huyo, aliishi naye kwake na alimpapasa matiti akilenga kumfanyia vitendo vya aibu.

Mwakasege amesema kuwa mshtakiwa huyo alimchukua mtoto huyo kutoka kwa wazazi wake Juni 2 hadi 04 mwaka huu alipokamatwa na kupelekwa Polisi.

Akijitetea mshtakiwa huyo amedai kuwa mtoto huyo hajamtorosha, bali alikutana naye mtaani baada ya kufukuzwa na wazazi na kuamua kumpa hifadhi kama Mtendaji.

Mshtakiwa amerejeshwa rumande kutokana na kukosa wadhamini na kesi yake itatajwa tena Julai 6 mwaka huu.


----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad