Kumbatio la Kajala na P Funk Lamtibua MKE wa P Funk..Atakiwa Kurudi Nyumbani Haraka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MJINI kuna mambooo! Juzi (Jumatano), Sinza jijini Dar es Salaam, kulikuwa na sherehe ya ‘bethdei’ ya msanii wa filamu nchini Kajala Masanja, lakini katikati ya shughuli likazuka jambo, tega sahani upakuliwe ubuyu.

Jambo lenyewe linamhusu prodyuza mahili Bongo, Paul Matthysse ‘P- Funk’ ambaye ni mzazi mwenzake na Kajala, kujikuta akipata ‘wenge’ baada ya kile kinachotajwa kuwa ni mkewe wa sasa (jina kapuni) kumaindi uwepo wake kwenye shughuli hiyo.

Baada ya kutimba kibabe kwenye sherehe hiyo, prodyuza huyo alikwenda moja kwa moja kwa EX wake na kumkumbatia ambapo ‘mama’ naye alionesha mahaba kwa kukata keki na kumlisha mzazi mwenzake.

Kitendo hicho cha P-Funk, kiliibua shangwe kwa wageni waalikwa waliokuwa wameshiriki shughuli hiyo iliyofanyika ndani ya ofisi ya Kajala iliyopo Sinza Afrikasana.

Hata hivyo, wakati shughuli ikiendelea, ghafla prodyuza huyo alipigiwa simu na mtu anayedaiwa kuwa ni mke wake akimhitaji arudi nyumbani.Chanzo cha karibu na P- Funk kiliwanong’oneza waandishi wetu kuwa, kuna wambeya kutoka shughulini hapo walikuwa wamerusha klipu ya video mtandaoni ikimuonesha Kajala na mzazi mwenzake huyo wakiwa wamekumbatiana jambo ambalo linadaiwa kumkera mke wa P- Funk.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad