AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kagera Inspekta Hamis Dawa, amesema kuwa taarifa za mwili wa mwanaume mmoja kuelea Ziwani zilitolewa na Padre Deritius Rwehumbiza wa Kanisa Katoliki Bunena mkoani humo ambalo liko jirani na Ziwa.
Inspekta Dawa ametoa kauli hiyo wakati akieleza taarifa ya Jeshi hilo, kuopoa mwili wa mwanaume mmoja ambaye bado hajafahamika anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 30 hadi 35, aliyezama ndani ya Ziwa Victoria na kisha mwili wake kuelea.
"Sasa hatujui kama ni mvuvi ama ni muogeleaji na sasa Ziwa letu limejaa sana na tumejaribu kutoa elimu kwa wananchi, kutowaachia watoto wao kwenda Ziwani" amesema Kamanda Dawa.
Imeelezwa kuwa mwili wa mwanaume huyo, umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na kuwataka wakazi wa Mkoa huo, kuacha mara moja tabia ya kuogelea Ziwani kwa sasa sababu Ziwa hilo limejaa sana.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK