WOLPER – Pesa za Kuhongwa Zina Mikosi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MKALImwingine kutoka uwanda wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper Massawe amesema, hakuna pesa zenye mikosi kama za kuhongwa na mwanaume.

Wolper amesema pesa za dizaini hiyo huwa zina mikosi mingi na mtu huwezi kuzifanyia kitu cha maana.

 

Akizungumza na Gazeti la IJUMAA WIKIENDA, Wolper amesema kuwa, zamani baadhi ya wanawake walikuwa wakifurahia pesa za kuhongwa, lakini ukweli ni kwamba hata ukitafuta mwanamke aliyefanikiwa kwa kuhongwa ni vigumu mno kumpata.

 

“Mimi mambo ya kusubiria pesa za kuhongwa, niliyafuta kabisa kwenye kichwa changu ndiyo maana nimekuwa na nguvu ya kufanya kazi zangu kwa umakini.

 

“Mimi pesa za kuhongwa sizitaki kabisa kwani zimejaa mikosi,” anasema Wolper.Staa huyo aliongeza kuwa, kazi yake ya ushonaji na kuuza vitenge kwenye duka lake lililopo Sinza-Makaburini jijini Dar, imemfanya kujulikana hadi nje ya nchi na pia anawaanda wasichana wengine wadogo waweze kujitegemea wenyewe na siyo kutegemea pesa za kuhongwa.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad