AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
JINA la Mbrazili, Marcio Maximo ni kati ya makocha 60 waliotuma maombi ya kuifundisha Yanga katika msimu ujao.
Yanga ipo kwenye mchakato wa kumpata kocha mpya atakayekuja kuinoa timu hiyo baada aliyekuwa kocha Mbelgiji, Luc Eymael kutimuliwa. Kocha mwingine anayetajwa kuwania kibarua cha Mbelgiji huyo ni Mfaransa, Patrick Aussems.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo limezipata Championi Jumatatu, Maximo amewasilisha maombi ya kuja kuifundisha timu hiyo.
Mtoa taarifa huyo alisema kuwa kocha huyo ametuma CV zake wiki iliyopita na kuungana na makocha wengine 59 walioomba kukinoa kikosi hicho.
Aliongeza kuwa uongozi wa timu hiyo umepanga kukutana wiki hii kwa ajili ya kupitia maombi na CV za makocha wote kabla ya kufanya mchujo. Maximo hivi karibuni aliliambia gazeti hili kuwa:
“Nipo tayari kujiunga na Yanga kama wakinihitaji, hivi sasa nipo nafundisha timu ya taifa ya Naguya iliyopo Amerika Kusini.”
WILBERT MOLANDI, Dar es Salaam
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK