Morrison alivyowajibu Yanga kuhusu kwenda FIFA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Baada ya Mwenyekiti wa Yanga Dkt. Mshindo Msolla kudai kuwa Jumatatu, Agosti 25 wanapeleka malalamiko yao rasmi FIFA juu ya utata wa mkataba wa winga Bernard Morrison, winga huyo ameibuka na kuwajibu.

Mwamba huyo kutoka nchini Ghana, kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram amewapiga kijembe waajiri wake wa zamani Yanga kwa kuweka picha akiwa na Kiungo Jonas Mkude inayoonyesha wanacheka, kisha akaandika kwa namna alivyosikia taarifa za kesi yake kufikishwa CAS na FIFA.



Morrison jana alionyesha thamani yake kwa kufunga bao pamoja na kutoa asisti kwenye ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Vital’o ukiwa ni mchezo wa Simba Day.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga Dkt Mshindo Msola alisema jana kuwa imemjumuisha Morrison kwenye usajili wao, jina lake wakiwa wamelisajili kwenye mfumo wa FIFA (TMS) kwa kuwa bado ni mali yao.



-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad