Obama amkosoa Trump kushindwa kudhibiti COVID-19

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama amemkosoa vikali Rais Donald Trump na serikali yake hapo jana juu ya namna alivyoshughulikia janga la ugonjwa wa COVID-19 nchini humo, wakati wa hotuba yake mbele ya wafuasi wa mgombea urais wa Democratic Joe Biden. 

Obama amesema Trump hawezi kuwalinda Wamarekani, wakati anashindwa hata kuchukua hatua za msingi kujikinga yeye mwenyewe, akimaanisha kulazwa kwa rais huyo hospitalini wiki kadhaa zilizipita baada ya kuambukizwa virusi vya corona. 


Kura za maoni ya umma zimeendelea kuonyesha kuwa Biden anaongoza kinyang'anyiro hicho cha urais dhidi ya Trump wa chama cha Republican. 


Aidha Obama amemkosoa Trump kwa kusema uwongo hadharani, pamoja na kushindwa kukemea tabia ya Wazungu kujipa hadhi ya juu nchini humo.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad