Bukoba Yatwaa Tuzo Anwani Za Makazi.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Manispaa ya  Bukoba Mkoani Kagera imepokea tuzo ya kutekeleza kwa ufanisi mradi wa anwani za makazi kwa kutumia fedha za ndani licha ya kuwa haikuwa kwenye mpango wa halmashauri zinazotekeleza mradi huo.


Taarifa iliyotolewa na mkurugenzi msaidizi huduma za posta kutoka wizara ya ujenzi,uchukuzi na mawasiliano Carolini Kanuth mjini Bukoba Novemba 16,Mwaka huu, amesema kuwa kufuatia kongamano lililofanywa na wizara hiyo waliamua kutoa tuzo kwa halmashauri ambazo zimetekeleza kwa ufanisi mradi huo.


Amesema kuwa zilichaguliwa manispaa mbili ikiwemo moja kutoka jiji la Mwanza ambapo ameeleza Manispaa ya Bukoba walianza kutekeleza mradi huo baada ya kupata mafunzo bila kusuburi pesa kutoka sehemu nyingine.


Akielezea umuhimu wa mradi huo kwa jamii,katibu tawala wa mkoa wa Kagera Prof. Faustine Kamuzora ambaye  ni muasisi wa mradi huo, amesema kuwa anwani za makazi zinarahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.


Kamuzora ameongeza kuwa uwepo wa namba kwenye nyumba pamoja na majina ya barabara na mitaa urahisisha huduma mbalimbali kama huduma za zima moto pale ajali hizo zinapotokea


Akielezea mpango uliopo kwasasa, kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Bukoba Japhet Kanoni amesema kuwa kwa mwaka 2020 na 2021, wametenga kiasi cha shilingi milioni 45 baada ya zoezi la majaribio la kuweka namba na vibao vya majina ya mitaa kufanikiwa.


Mpaka sasa katika manispaa ya Bukoba tayari barabara 100 zimetambuliwa kwa kuwekewa vibao zikiwemo nyumba 49


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad