Idadi ya vifo vya corona Ulaya yapindukia 400,000

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Zaidi ya watu 400,000 wamefariki dunia kutokana na maambukizi ya virusi vya corona barani Ulaya kulingana na takwimu za leo zilizokusanywa na shirika la habari la AFP, kutoka katika vyanzo rasmi vya kuaminika. 
Bara la Ulaya ni la pili liloathiriwa vibaya na maambukizi ya virusi hivyo baada ya Amerika Kusini na Karibiki. 

Watu wapatao 400,649 wamefariki kutokana na ugonjwa wa COVID-19. Idadi hiyo ni kutoka miongoni mwa watu 17,606,370 waliothibitishwa kupata ugonjwa huo barani humo. 

Vifo 36,147 vimetokea katika wiki chache zilizopita. Inatajwa kuwa ni idadi kubwa zaidi ya vito kutokea barani Ulaya tangu janga hilo la maambukizi kuanza mwanzoni mwa mwaka. 

Nchi zinazoongoza kwa kuwa na maambukizi mengi ni Uingereza, ikifuatiwa na Italia, Ufaransa, Uhispania pamoja na Urusi.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad