IGP Sirro azungumzia yanayoendelea Mtwara

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania IGP Sirro amesema Jeshi la Polisi litachukua muda mfupi kukabiliana na uhalifu unaoendelea katika Mkoa wa Mtwara, kama ilivyofanya katika kukabiliana na mauaji ya raia katika Wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani.

 

IGP Sirro amesema hayo wakati akizungumza na wakazi wa Kitava mkoani humo, ambapo ameahidi kuwa tatizo hilo halitachukua muda mrefu kwani vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kutokomeza uhalifu huo waliohusika na matukio ya utesaji raia na uharibifu wa mali zao wanachukuliwa hatua.


“Wananchi wetu wamepata shida na waliofanya shida lazima washughulikiwe kwa mujibu wa sheria zetu kwa kushirikiana na Msumbiji sababu wana taarifa watu wanaotoka huko kuja kufanya Tanzania,” amesema IGP Sirro.


 IGP Sirro ameongeza kuwa, “Kimsingi ni kwamba, tumejipanga vizuri wananchi wetu waendelee kurudi kwenye yale maeneo waliyokimbia kule mpakani (mpakani mwa Tanzania na Msumbiji), tumeshajiimarisha, tutahakikisha hili tatizo litachukua muda mfupi kama ilivyokua kwenye tatizo la Kibiti na Ikwiriri ilivyochukua muda mfupi. Hawa wahalifu tutawashughulikia huko huko waliko”.

VIDEO:


----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad