Pigo jingine kwa Liverpool hili hapa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Nahodha wa klabu ya Liverpool, Jordan Henderson amepata maumivu kwenye mguu wake wa kulia na kushindwa kuendelea na mchezo wakati timu yake ya Taifa Uingereza ikicheza dhidi ya timu ya Taifa ya Ubeligiji na Uingereza Kufungwa mabao mawili kwa sifuri usiku wa hapo jana.

Maumivu aliyopata Jordan Henderson yanafanya orodha ya wachezaji wanaotumainiwa kwenye klabu ya Liverpool kufika tisa na kuzidi kumpasua kichwa kocha wa klabu hiyo Jurgen Klopp wakati akijiandaa kuwavaa Leicester City kwenye mchezo wa EPL Unaotaraji kuchezwa Jumapili ya wiki hii.




Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, Gareth Southgate amesema “Ni kweli Jordan amepata maumivu ya mguu na akahisi hawezi kuendelea na mchezo lakini hana uhakika kama ni kuchanika kwa nyama za paja”. Lakini atafanyiwa vipimo zaidi baada ya timu kurejea Uingereza, Aliongezea Southgate.




Wachezaji nyota tisa wa Liverpool wanaosumbuliwa na majeraha ni walinzi wote wa chaguo la kwanza, Virjil Van Dijk, Joe Gomez, Andy Robertson na Trent Alexander Anorld.

Viungo Fabinho, Thiago Alcantara, Alexander Oxlade Chamberlin na mshambuliaji Mohammed Salah ambaye ameripotiwa kupata maambukizi ya Ugonjwa wa Korona.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad